Baada Ya Kutumbuliwa Cheo Chake Cha IGP......Ernest Mangu Apewa Cheo Hiki Kizito Soma Hapa
Rais John Magufuli amemteua aliyekuwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, huku aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Mangu akiteuliwa kuwa balozi.
Rais Magufuli Mei 28,2017 alitengua uteuzi wa IGP Mangu na kumteua Simon Sirro kushika wadhifa huo.
Mangu anasubiri kupangiwa kituo cha kazi pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dk Aziz Mlima.
Uteuzi wa Rais Magufuli, uliotangazwa Alhamisi Oktoba 26,2017 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi uliwahusu pia, makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na wakuu wa mikoa ambao wataapishwa Ijumaa Oktoba 27,2017 mchana Ikulu jijini Dar es Salaam.

Comments
Post a Comment